Kuhusu Yohana mbatizani.006Ubtz3.17jan17.4-8

.4/8.!!!Kuhusu Yohana mbatizani.!!!

.i/viii. Hakuwa mtu mdogo“†††lakini ni mdogo sana†††”.

Math 11:11 Amin, nawaambieni, Hajaondokea mtu katika wazao wa wanawake aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; walakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.

.ii/viii. Mfalme Herode alimwona Yesu kuwa ni kama Yohana Mbatizaji.
Math 14:1 Wakati ule mfalme Herode alisikia habari za Yesu, akawaambia watumishi wake,    2 Huyo ndiye Yohana Mbatizaji; amefufuka katika wafu; na kwa hiyo nguvu hizo zinatenda kazi ndani yake.+ Marko6:14.

.iii/viii.  Na yeye Herode ndo ali mwuaga.
Math 14:8 Naye, huku akichochewa na mamaye, akasema, Nipe hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji. + Marko 6:24.


.iv/viii. Watu wengine pia walimwona Yesu kuwa ni Yohana Mbatizaji.
Math 16:14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii. + Marko 8:28, Luka 9:19.


.v/viii. Yohana Mbatizaji alionekana kuwa na pepo.
Luka 7:33.
“†††33 Kwa kuwa Yohana Mbatizaji alikuja, hali mkate wala hanywi divai, nanyi mwasema, Ana pepo. 34 Mwana wa Adamu amekuja, anakula na kunywa; nanyi mwasema, Tazama, mlafi huyu, na mnywaji wa divai, rafiki wao watoza ushuru na wenye dhambi.†††”

.vi/viii. Na huyo Yohana mbatizaji ndiye Eliya.

Math 17: 10 Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza?   11 Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote,     12 ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao.     13 Ndipo wale wanafunzi walipofahamu ya kuwa amesema nao habari za Yohana Mbatizaji.
“†††
.1.     Wanafunzi wa Yesu hawakujua kama yeye ni Eliya.
.2.     Wanafunzi wa Yesu waliuliza maswali na hawakujitia ujuaji na kukaa kimya bali walijitia ujuaji kwa kujua kutoka kwa mjuaji (mwalimu wao) Yesu.
.3.     Yesu alikuwa anajibu maswali aliyoulizwa.
.4.     Petro alipomwona (Math 17:4) alimtambua kuwa ni Eliya ila si kama Yohana Mbatizaji ijapokuwa Eliya alikuwa wa zamani sana kuliko Yohana Mbatizaji.
.5.     Yesu aliwajuza kuhusu walilouliza baada ya kuuliza, maana nao wasingeliuliza, hata wao wasingelijua kama waliyemwulizia. †††”


.vii/viii. Yohana kutamka kwa uwazi kuhusu kupinga ubatizo wa maji.

Math 3:11 Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
==>> Marko 1:8, Luka 3:16, Yohana 1:26.

“†††.viii/viii. Yohana Mbatizaji hakujitambua kuwa yeye ni Eliya.
Yohana Mbatizaji asema yeye si Eliya.
Yoh 1:
18
Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.
19
Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?
20
Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.
21
Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La.
22
Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako?
23
Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya.
24
Nao wale waliotumwa walikuwa wametoka kwa Mafarisayo.
25
Wakamwuliza, wakamwambia, Mbona basi wabatiza, ikiwa wewe si Kristo, wala Eliya, wala nabii yule?
26
Yohana akawajibu akisema, Mimi nabatiza kwa maji. Katikati yenu amesimama yeye msiyemjua ninyi.
27
Ndiye yule ajaye nyuma yangu, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya kiatu chake.
28
Hayo yalifanyika huko Bethania ng'ambo ya Yordani, alikokuwako Yohana akibatiza.
:21 - Yohana alipoulizwa kuhusu kama yeye ni Eliya amesema, “mimi siye” na aya ya :25.

Maelezo ya aya zingine, katika Yohana 1:
.01.    :18 - Yesu ni Mungu mwana (utatu)
.02.    :20 -  Yohana asema yeye si Kristo.
.03.    :20 -  Yohana asema yeye si Eliya.
.04.    :20 -  Yohana asema yeye si Yesu (nabii yule :27) niweke ___ rejea zingine).
.05.    :22 – Watu walimjia Yohana kumwuliza maswali naye aliwajibu.
.06.    :23 - Yohana ni sauti ya mtu aliaye nyikani.
.07.    :23 - BWANA ana njia ambayo ni jukumu lako mwanadamu kuinyosha.
.08.    :23, :27 - Yohana alikuwa anaijua historia na pia anayathamini maneno ya manabii.
.09.    :23, :27 - Neno la Mungu litatimia/linatimia/li hai.
.10.    :23, :27 - Neno la BWANA lina wakati wake.
.11.    :23, :27 - Biblia ilikuwa inasomwa.
.12.    :24 - Mafarisayo walikuwa wadadisi.
.13.    :25 – Ilifahamika dhahiri kuwa ubatizo utakuwepo.
.14.    :25 - Mafarisayo walifahamu kuwa mbatizaji ni Kristo au nabii yule au Eliya na si nje ya hapo.
.15.     :26 - Yohana asema, 'mimi nabatiza’ si ‘Yesu kupitia mimi’.
.16.     :26 - Mafarisayo walikuwa hawamjui Kristo wala nabii yule.
.17.     :27 - Yesu ndiye ajaye nyuma ya Eliya na pia inaonesha kuwa Yohana ni Eliya..

Angalia usiwe kama mafarisayo. Wao neno wanalijua lakini hawamjui aliyesemwa kwenye neno.
Hivyo ndivyo Biblia ime/ilivyomwelezea Yohana.†††”
















(sehemu hii bado inafanyiwa marekebisho) 


Lesson Series

Downloads
.1.
006Ubtz3.17jan17.1/8
Maana ya ubatizo.

.2.
006Ubtz3.17jan17.1/8


.3.
006Ubtz3.17jan17.1/8


.4.
006Ubtz3.17jan17.1/8


.5.
006Ubtz3.17jan17.1/8


.6.
006Ubtz3.17jan17.1/8


.7.
006Ubtz3.17jan17.1/8


.8.
006Ubtz3.17jan17.1/8


.9.
Complete Ubatizo 3.   (hakuna bali ipo ubatizo 2 ambayo ni complete, kupata Ubatizo 2 bonya hapa)




Comments