Malumbano kuhusu ubatizo (kwa maji) 006Ubtz3.17jan17.2-8

.2/8..!!!Malumbano kuhusu ubatizo (kwa maji)!!!.
(bila kujali ni maji machache au mengi)
Ukitaka kujua hakuna haja ya kulumbana kuhusu ubatizo wa/kwa maji, jiulize na ujijibu.

Musa, Ayubu, Abramu (si Abrahamu)/Ibrahimu, Enoko,Eliya, Elisha, n.k. hao ni baadhi ya watumishi fulani wa Agano la kale. †††Je, walikuwa watumishi wadogo au wakubwa?!...


Je, walibatizwa?!.  Je, kati ya hao, akinanani walimtokeaga Yesu? mara ngapi (kuonesha wapo hai)?!. Je, walibatizwa?!.

†††Mathayo 17, Marko 9, Luka 9,
Mathayo 17:
1
Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;
2
akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang'aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3
Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.
4
Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya.
5
Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.
6
Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana.
7
Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope.
8
Wakainua macho yao, wasione mtu ila Yesu peke yake.
9
Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu.
10
Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza?
11
Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote,
12
ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao.
13
Ndipo wale wanafunzi walipofahamu ya kuwa amesema nao habari za Yohana Mbatizaji.

“†††Katika aya hizo tunaona mengi:-
.1.   :1 - Kuna wakati Yesu alijitenga na kubaki na  wanafunzi wake tu.
.2.    :3 - Musa na Eliya kumtokea Yesu.
.3.    :4 - Petro alimwona/aliwaona Musa na Eliya.

.4.    :4 - Petro aliwatambua Musa na Eliya.
.5.    :8 - Musa na Eliya ni watu.


.6.    :9 - Hayo yalikuwa ni maono.
.7.    :9 - Yesu ni wa mipango katika wakati wa utimilifu.
.8.    :9 - Yesu alijua kuwa atafufuka katika wafu; maana yake alijua kuwa atakufa (Math 16:23-Petro aliona si vyema kufa kwa Yesu, basi Yesu akamwita Petro ‘Shetani’).

.9.    :9 - Yesu ni mwana wa Adamu.
.10.     :10 – Wanafunzi wa Yesu walikuwa wanafahamu historia ya kale.


.11.     :10 – Wanafunzi wa Yesu walikuwa wanauliza/wanamwuliza Yesu.
.12.     :10 – Wanafunzi walitambua/walimtambua Yesu kuwa yeye si Eliya.
.13.     :10 – Wanafunzi hawakutambua kuhusu kuja kwa Eliya kutatimia lini ila kutatimia kabla ya Yesu/ kutatimia na ndo atakuja Yesu.

.14.     :10 – Wanafunzi walitambua/walimtambua Yesu kuwa alitabiriwagwa/alitabiriwaga na ndo wakonaye (mwalimu wao).
.15.     :10 – Wanafunzi walitambua/walimtambua Yesu kuwa yeye si Eliya na wakamhoji/wakamuuliza.


 .16.    :10 – Yesu alikuwa akiwajibu wanafunzi wake maswali. (kwakuwa Yesu alikuwa mwalimu wao?).
.17.     :10 – Wanafunzi wa Yesu walijua kuwa Yesu atakuja na ameshakuja na ndo huyo waliyenaye pamoja, ila kabla yake Yesu kuna ambaye alipaswa kuja/kutangulia. Sasa ndo wanaona kuwa huyu Yesu nikama amekuja kabla ya aliyetabiriwa. Yaani waliona kama unabii umepishana/umepingana.
.18.     :11 - Yesu hujibu kwa ufasaha kwa kukubali kinachopaswa kukubaliwa.

.19.     :11 - Yesu aliijua historia.
.20.     :11 - Eliya alikwisha kuja (kurudi) kabla ya Yesu.
.21.     :12 - Labda Eliya alipokuja hakusemaga kuwa yeye ni Eliya na kwakutokana na hilo, ndo maana walimtenda walivyotaka na pia wanafunzi hawakujua/hawakumtambua.
.22.     :13 - Wanafunzi wa Yesu waerevu sana.


Kuhusu kutokuwepo na ubatizo miaka ile, †††”

Yeye Yohana Mbatizaji, yupo mbinguni au laa?!. Je, alibatizwa?!. Je, kabla ya Yohana kulikuwa na ubatizo?!. Kama haukuwepo, waliendaga wapi?!. Au basi hakuna umuhimu wa ubatizo kama bila kubatizwa unaenda Mbinguni maana imeonekana wameenda mbinguni.

“†††Manabii wa miaka ile:-
.1. Isaya. .2. Yeremia. .3. Musa. .4. Miriamu. .5. Debora n.k. Walibatizwa?!...

Wafalme:-
.1. Samweli. .2. Sauli. .3. Sedekia. .4. Daudi. .5. Sulemani n.k, je, walibatizwa?!...

Bila kujali ni maji mengi au kidogo au machache au makubwa, je, walibatizwa?!...

Kama hawakubatizwa na Mungu alikuwa pamoja nao na aliwatumia, Je, si kwako / kwetu?!... au wewe unataka ubatizwe tu na Mungu asiwe nawe au  uwe na Mungu bila kubatizwa au vyote?!...

Kwa kufikia hapo, sioni haja ya kugombana kuhusu kiasi au kiwango cha maji ila kuhusu maji ujue kuwa Yesu ni maji yaliyohai.


-->Mtu anajitetea kwa kusema, ‘hao sawa hawakubatizwa, ila Yesu alibatizwa’.
 Sawa. Sasa hao pia walioa ila Yesu hakuoa. Hao pia hawakusali kanisani, Yesu naye hakusali kanisani basi na wewe usisali kanisani. Hao pia hawakutumia Biblia ya agano jipya na Yesu pia, basi na wewe pia. Hao pia … Umechagua unaloweza ukalifanya kwa kuliiga na kulifanya, basi sawa, unashangaa kwangu nikichukua linalonifaa na kulifanya?!...
Sioni haja ya kulumbana.
Kama unahoja zaidi wasiliana nasi/nami. †††”





Comments