Daily Bread? (Neno la Kila siku?)
S/N
|
Verse
|
Word
|
1
|
||
2
|
||
3
|
||
4
|
Isaya 9:6a
[6]Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; |
|
5
|
Kumbukumbu la Torati 11:26-28
[26]Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana; [27]baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, niwaagizayo leo; [28]na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, mkikengeuka katika njia niwaagizayo leo, kwa kuandama miungu mingine msiyoijua. |
|
6
|
Ukristo katika Biblia.
Matendo ya Mitume 11:26 [26]'c' Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia. Ni Mara ya kwanza kabisa kuitwa '.....'. |
|
7
|
Hesabu 6:24-26
[24]BWANA akubarikie, na kukulinda; [25]BWANA akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili; [26]BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani. |
|
8
|
Kutoka 1:12
[12]Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea. Nao walichukiwa kwa sababu ya wana wa Israeli. |
|
9
|
Panua Mahali pa:-
1. Biashara yako 2019 2. Uchumi wako 2019 3. Elimu yako 2019 4. Upendo wako 2019 5. ... Ni wewe ndo ufanye, so Mungu akufanyie. Isaya 54:2. |
|
10
|
Ufunuo wa Yohana 21:1
[1]Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapanak bahari tena. Kuna muda:- Utapita na vyake. Kuna vitu ambavyo lazima viondoke ndo vije vingine. |
|
11
|
Mathayo 11:28
[28]Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. |
|
12
|
||
13
|
Moja ya sifa za Biblia ni:- Kujibu.
Zaburi 119:9 a-Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Jibu: b-Kwa kutii, akilifuata neno lako. Je, Unaswali?. |
|
14
|
Yakobo 1:12
Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao. Tafakari kushinda majaribu. |
15
|
Waefeso 3:20
[20]Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu; |
|
16
|
Yakobo 4:7-8
[7]Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. [8]Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili. |
|
17
|
Yakobo 4:13-16
[13]Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; [14]walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka. [15]Badala ya kusema, Bwana akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi. [16]Lakini sasa mwajisifu katika majivuno yenu; kujisifu kote kwa namna hii ni kubaya. |
|
18
|
Neno la Leo.
Yoshua 24:15 A-Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia BWANA, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; B-kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; C-lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia BWANA. Amin. |
|
19
|
"Usipende usingizi usije ukawa maskini; ..." Mithali 20:13'A. Ni moja ya sifa ya Biblia kuwa, Inashauri. Nakutakia usiku mwema. |
|
20
|
"Kila siku, Bwana hutuhurumia."
Maombolezo 3:22-23 [22]Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi. [23]Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu. Jua, kila siku, Bwana ameshatuandilia fungu jema, "rehema". Amina. |
Comments
Post a Comment